Wednesday, July 13, 2011

Baadhi ya wakazi wa jimbo la Musoma Mjini nao wataka posho ziondolewe

Baadhi ya wakazi wa Jimbo la Musoma Mjini mkoani Mara, wameungana na Chadema na kuitaka serikali kuondoa posho za wabunge, watumishi wake na kuachana vikao visivyo na tija ili fedha zielekezwe katika matatizo ya msingi.
Vicent Nyerere ambaye ni mbunge wa jimbo hilo kwa tikati ya Chadema ndiye aliyesema hayo akiwakariri wakazi wa jimbo lake waliimpa ujumbe huo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mara Sekondari.
Nyerere alisema wananchi wakazi hao walimwambia hayo kwenye mkutano wake alioutisha mjini humo ili wamweleze kero  zinazowabili na yeye mwenyewe (Nyerere) kuwaleleza utekelezaji wa baadhi ya miradi ya maendeleo.
Wakazi wa jimbo langu wanataka fedha zielekezwe kwenye huduma za kijamii na kwa upande wa elimu na afya ambako ndiko kwenye matatizo mengi ambayo hadi sasa hajapatiwa ufumbuzi," alisema Nyerere.
Mbali na hilo, alisema kuwa wakazi wa jimbo lake pia walimuomba apeleke ujumbe kwa serikali kwamba  wanataka kujua kwa nini mafuta yanaendelea kupanda bei wakati serikali ilishatangaza kuwa kufikia Julai mosi yangeshuka bei.
Aidha, alisema kuwa katika mkutano huo aliagiza wafanyabiashara wote ambao wamepewa vibali vya kununua mahidi kwenye ghala la taifa Shinyanga ili kukabiliana na njaa jimboni humo wayapeleke haraka.
Alisema wapo baadhi yao wameingia mitini huku mmoja wao akiwa amepewa kibali vya kuleta tani 100 za mahindi ambapo amemwagiza eleta mahindi ama arudishe kibali kabla ya kukumbana na mkono wa sheria.
"Jimbo langu lina kata 13 kama wafanyabiashara waliopewa vibali wangefikisha mahindi kwa wakati, makali ya njaa yangepungua, lakini ujanja huu unaofanywa na baadhi ya wafanyabishara unachangia kuwepo kwa njaa," alisema.
Nyerere pia alikagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kuangalia kama fedha zilizotolewa zikitumika ilivyotakiwa na ameona hakuna ufisadi uliofanyika na kwamba kila kitu kilifanyika vizuri.
Mbunge huyo aliitaja baadhi ya miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa barabara, madaraja na ukarabati wa madawati ya shule za msingi na kufunga madampo likiwemo la soko la Nyakato mjini humo.
Katika hatua nyingine, Nyerere alisema kuwa ujenzi wa maabara ya kisasa itakayotumiwa na shule tano za sekondari za kata zilizojengwa kwenye kata moja jimboni humo, unatarajia kuanza hivi karibuni.
Alisema ujenzi huo utaanza kufuatia mfuko wa jimbo kuwa na jumla ya shilingi milioni 34 na kwamba awali mfuko huo ulikuwa na shilingi milioni 17 ambapo zimeongezeka nyingine milioni 17 na kufikia milioni 34.
Alisema kuwa fedha hizo zitatosha kujenga jengo la maabara, kuweka meza na viti na kwamba ataendelea kusubiri nyingine ambazo zitatumika kununulia vifaa vya maabara ili wanafunzi waanze kuitumia.

No comments:

Post a Comment